Archive Page

Kwa miaka mingi iliyopita, shule na jamii zimekuwa zikishiriki malengo ya kufunza maadili na tabia nzuri kwa vizazi vijavyo. Tabia ambazo zimekuwa zikipewa uzito kwa watoto na hata waliobalehe na kuvunja ungo ni pamoja na uajibikaji, ujasiri, haki, uaminifu, heshima na kujithibiti. Kwa muda mrefu, imekisiwa kuwa juhudi hizo zingeboresha hali ya binadamu na hata kutoa maana pana zaidi kuhusu maisha na kukuza hadhi ya utu wa watu wote. Maadili ya ngono pia yalijumuishwa kwenye mafunzo ya maadili yaliyofunzwa sana ya kutoshiriki ngono hadi siku ya ndoa. Hiki ndicho kiwango kilichotarajiwa kudumishwa.

Lakini mabadiliko ya tamaduni miaka ya 1960 na 1970 –ambayo huitwa mapinduzi ya ngono - yalichangia kuibua maswali mengi kwa umma, na hata maadili hayo kutupiliwa mbali. itikadi hii iliwaruhusu watu wawe na uhuru wa kushiriki ngono bila mipaka ya ndoa, bila mahusiano na hata bila upendo. Filamu, muziki, televisheni, majarida na vyombo vingine vya habari vikipigia debe dhana hii kwa uwazi. Kwamba ngono na yeyote–bila ndoa ama hata bila mahusiano –ni kawaida na jambo la kuvutia mradi tu mmekubaliana, na hakuna anayepata mimba ama kuambukizwa ugonjwa wa zinaa.

Dhana mpya ya uhuru wa ngono haikuleta furaha kama ilivyodhaniwa, bali kudorora kwa maadili ya watu binafsi na jamii kwa ujumla. Ongezeko la visa vya talaka, mimba za vijana ambao hawakuolewa, uavyaji na familia za mzazi mmoja ziliongezeka. Kuongezeka kwa maradhi ya zinaa yakiwemo yale ambayo hayakujulikana kwenye vizazi vya awali yamefikia kiwango cha kuwa majanga na mara nyingi yana athari za kudumu au hata kifo.

Katika kukabiliwa na hali hii ya kutisha, mashirika ya elimu, serikali na vitengo vya afya ya umma wamejbu kwa mafuriko ya jumbe za kupunguza hatari zinazojulikana kama Kupunguza Hatari ya Ngono zinazolenga vijana na vijana wazima. Jumbe hizi zinalenga njia za kupunguza uwezekano wa kupata mimba ama kuambukizwa magonjwa ya zinaa kwa kuendeleza utumiaji wa mipira ya ngono (kondomu) badala ya kuangazia na kushughulikia suala la kutoshiriki ngono kabla ya ndoa.

Kuna mijadala na majadialiano kuhusu elimu gani ya ngono vijana wapewe ili kukabiliana na haya maendeleo ya kutisha.Hasa zaidi, kama wanapashwa kufundishwa juu ya kutoshiriki ngono kabla ya ndoa [KUEPUKA Hatari ya Kujamiiana] au kupunguza uwezekano wa kupata mimba au kuambukizwa magonjwa ya zinaa kwa kukuza njia za kuzuia mimba hasa kondomu [KUPUNGUZA Hatari ya Ngono]

Wengine wanaamini kwamba vijana wanapaswa kuelimishwa kuhifadhi shughuli za ngono kwa ajili ya ndoa tu. Wanao wasiwasi kwamba kuwafundisha vijana kuhusu mambo ya kuzuia kupata mimba kutawafanya wafanye ngono kabla ya wakati wake (k.m., Elimu ya kutoshiriki Ngono Nje ya Ndoa).

Wengine wana maoni kwamba vijana watafanya ngono kwa vyovyote vile na lazima waelekezwe jinsi ya kuepuka mimba za nje ya ndoa na kujikinga na magonjwa ya zinaa; kwa hivyo wanaiona elimu ya kujiepusha na kutoshiriki ngono nje ya ndoa kuwa si ya kweli na haiendani na wakati tuliopo sasa (k.m., Ngono Salama au Elimu Kamili ya Ngono)

Mtazamo wa kufikiria kwa suala hili unapaswa kuzingatia zaidi walengwa wa elimu ya ujinsia: vijana wenyewe.

Ubongo Wa Vijana (Waliobalehe/Kuvunja Ungo)

Uchunguzi umeonyesha kwamba ubongo wa mwanadamu hukamilisha ukuaji wake kikamilifu kati ya umri wa miaka 25 na 30. Kwa hivyo, watoto wetu bado hawana uwezo wa kimantiki wa kiakili wa kufanya maamuzi ya ukomavu au ya busara mpaka wanapofikia zaidi ya miaka ya 20, kwa sababu mfumo wao wa ubongo wa kihisia unakomaa kabla ya ubongo wa busara.1

Wakikabiliwa na mihemko na tamaa wanazopitia kwa nguvu wakati wa ujana, kuna uwezekano kwamba vijana wanaweza kutotathmini kwa usahihi hatari na matokeo ya matendo yao.2 Wanapojikuta katika hali zenye msukumo wa kihisia, mfumo wao wa viungo uliokomaa zaidi hushinda mfumo wao wa udhibiti ambao haujakomaa, na hii huongeza uwezekano wa wao kujihusisha na tabia za hatari. 3.

Vijana Wanahitaji Wazazi na Washauri Wanaoaminika

Kwa sababu ya ukuaji wao wa kinyurolojia, vijana wanahitaji usaidizi wa wazazi na walimu au watu wazima wanaoaminika ili kujifunza jinsi ya kufanya maamuzi ya busara kupitia mwongozo unaorudiwa, wazi na thabiti. Wazazi, haswa, wanapaswa kuwa watu wa msingi kufundisha watoto wao elimu ya ngono, kulingana na maadili ya familia zao (ambayo ni pamoja na mila za imani, ikiwa zipo).

Wazazi wana masilahi bora ya watoto wao moyoni, wanaelewa ni nini watoto wao wako tayari kujifunza, na wao ndio mahali pa usalama pa kuanzisha na kuendeleza mazungumzo kuhusu ngono katika muktadha wa uhusiano salama wa mzazi na mtoto. Kinyume na imani maarufu, katika uchunguzi wa vijana 6,500, 79% yao wanasema kwamba wazazi wanapaswa kuwa chanzo cha msingi cha elimu ya ngono, shule (7%), mtandao (1%) na marafiki (1%). - ingawa kwa uhalisi ni 13% pekee waliotaja wazazi kama chanzo kikuu cha habari za ujinsia4.

Vijana Wanahitaji Ushawishi Mzuri wa Vijana wa Rika Lao

Vijana wenzao pia wanaweza kuwa na athari kubwa kwa tabia ya ngono ya vijana-kwa uzuri au ubaya. Uchunguzi umegundua kuwa wanafunzi walio na marafiki wanaotumia vitu visivyo vya halali au pombe huwa na tabia ya kuongeza matumizi hayo, lakini wale wanaoshiriki katika programu zinazoongozwa na wenzao ili kupunguza matumizi ya vileo au pombe wana uwezekano mkubwa wa kupunguza matumizi hayo.5,6Tabia ya kushiriki ngono nayo ni vivyo hivyo pia. Kwa hakika, vijana wanapotambua kwamba wa rika lao wanashiriki tendo la ndoa, uwezekano wa kufanya hivyo wao wenyewe ni mkubwa,7 kushiriki ngono mara yao ya kwanza inafanyika wakiwa umri mdogo zaidi. 8 Uhusiano huu wa mtazamo wa vijana kuhusu tabia ya ujinsia ya wenzao na tabia zao za ngono ni wa kweli, hasa kwa wavulana, na hii ni kweli katika tamaduni mbalimbali.9

Kwa kuelewa ukuaji wa ubongo, haishangazi kwamba vijana hupitia mahangaiko zaidi wakihisi kwamba watatengwa au kutohusishwa na wenzao. Wanaweza kutenda matendo fulani ili kuepuka hisia hiyo. Wanapojitambua zaidi katika hatua hii, pia wanakuwa na wasiwasi kuhusu kile ambacho wengine wanawafikiria, jambo ambalo linaweza kuwafanya kuwa hatarini kwa aina fulani za ushawishi mbaya 2

Vijana Wanahitaji Mwongozo

Vijana wanahitaji maono ya faida za kusubiri kushiri ngono mpaka kwenye kujitoa katika mahusiano ya ndoa. Kuna ushahidi mwingi wa kuthibitisha athari chanya ya kisaikolojia na ustawi kwa wale wanaohifadhi ngono kwa ajili ya ndoa.10, 11 Kujulikana na kupendwa kikweli katika ndoa ya kudumu ni uhuru wa kweli na huleta ukuaji na kustawi kwa mwanadamu.

Vijana wanahitaji ujuzi, mikakati, nguvu ya tabia na usaidizi ili kujiepusha na shughuli za ngono kabla ya wakati. ili kuepuka shughuli za ngono kabla ya wakati, vijana wanahitaji ufahamu wa hatari na athari za shughuli za ngono kabla ya ndoa kwao wao wenyewe na wengine katika suala la afya ya mwili, ustawi wa hisia, na tabia wanayoijenga maishani. Madhara ya shughuli za ngono za vijana ni pamoja na mimba zisizotarajiwa, magonjwa ya zinaa, maumivu ya kihisia na matatizo yanayoweza kujitokeza katika mahusiano ya baadaye.

ikiwa ujumbe unaohimiza kujiepusha na ngono hadi ndoa unafaa, hauwezi kutegemea tu kauli mbiu za “sema hapana” au madarasa ya mara moja moja ya elimu ya afya kuhusu magonjwa ya zinaa. Ni lazima ujumbe huu uimarishwe kwa njia mbalimbali—nyumbani, shuleni, na katika jumuiya. Familia, shule, jumuiya za dini, mashirika ya vijana, serikali na vyombo vya habari lazima kufanya juhudi za makusudi, na kushirikiana kwa umakini ili kujenga tabia ya vijana wetu. Shule ambazo zinatoa elimu ya kujenga tabia kwa umakini, thabiti na kwa kina na upana, huonyesha mienendo ya wanafunzi iliyoboreshwa, jumuiya ya kistaarabu na inayojali, na utendaji wa masomo ulioboreshwa.

Hata wafanya biashara na vikundi vingine vya kijamii vinapaswa kuwasaidia vijana kujenga aina ya tabia ambayo itawawezesha kuwa wafanyakazi waaminifu na wenye tija, majirani wema, wenzi na wazazi wanaojali, na raia wanaowajibika.

Elimu ya Ujinsia Inayowazingatia Vijana

Kwa kuwa vijana huelekea kupata ugumu zaidi kuliko watu wazima kufanya maamuzi yenye mantiki katikati ya mihemko na matamanio yenye nguvu, jinsi gani elimu ya ujinsia inaweza kuwasaidia vijana kuepuka kuwa na hisia zao zenye nguvu za ngono kuwaongoza kufanya maamuzi ambayo watajutia baadaye?

Kwa kuzingatia mahitaji ya vijana ambao wanaendelea kukua, aina ya elimu ya ujinsia ambayo inawahudumia vyema zaidi ni ile inayoweza kuwapa—pamoja na jumuiya ya wenzao—taarifa na mahusia yanayofaa na yanayolingana na umri wao. Elimu ya ujinsia inayowazingatia vijana inapaswa kulenga kukuza akili zao kijinsia ili waweze kufanya maamuzi mazuri kuhusu ngono ambayo yatawanufaisha wao na wengine, katika muda mfupi na kwa muda mrefu. Kwa hakika, elimu ya jinsia inayowawezesha kuahirisha kujamiiana kwa mara ya kwanza hadi umri wa baadaye, wakati wanaweza kuelewa kikamilifu matokeo ya maamuzi yao, italeta matokeo bora zaidi kwa vijana.12

Mafundisho ya Jumla kuhusu Uzazi wa Mpango

Wale wanaotetea ufundishaji wa vijana kutumia uzazi wa mpango wanajali kuwalinda dhidi ya magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa. Hebu tuangalie itumikayo zaidi kwa uzazi wa mpango-kondomu. Mbinu hii ina ufanisi gani?

Kwa hivyo je, kufundisha vijana kimakusudi jinsi ya kutumia kondomu kutahakikisha matumizi yao thabiti na sahihi, au kuna athari isiyotarajiwa ya kuwatia moyo kujihusisha na tabia ya kushiriki ngono na hatari zake kutokana na kwamba akili ya busara haijakomaa bado? Kuna jambo linaloitwa fidia ya hatari: Watu huwa na tabia ya kupunguza uangalifu wao na wako tayari zaidi kujihusisha na tabia hatari wanapoamini kwamba hatari yao imepunguzwa na teknolojia.19 Kwa mfano, watu wanaotumia mafuta ya kujikinga na jua huwa wanakaa muda mrefu kwenye jua20 na vifo vinavyohusiana na magari barabarani viliongezeka baada ya sheria za ulazima wa kuvaa mikanda ya usalama kuanzishwa.21 Hisia ya kupungua kuathirika husababisha kuongezeka kwa tabia ya kutojali. Pia kulikuwa na utafiti wa hivi majuzi ambao ulionyesha mabadiliko katika tabia ya hatari ya kujamiiana. Baada ya miezi sita ya matibabu ya kuzuia VVU (kabla ya kuambukizwa), ilisababisha matukio ya kuongezeka kwa magonjwa ya zinaa kupitia fidia ya hatari ya tabia.22

Vile vile, elimu ya ujinsia ambayo ina msisitizo wa kukuza matumizi ya kondomu inaweza kuongezeka bila kukusudia-badala ya kupunguza-shughuli za ngono (ikiwa ni pamoja na wapenzi wengi) na udhihirisho wa ngono usio salama (kutokana na kutofautiana na utumiaji usio sahihi, au “kutojali,” kati ya vijana.23, 24

Kwa maneno mengine, elimu ya ujinsia ambayo inazingatia matumizi ya uzazi wa mpango, iliyounganishwa na uwezo mdogo wa vijana wa kutathmini hatari kwa usahihi, inaweza kusababisha vijana:

Tunahitaji kukiri kwamba katika enzi hii ya kidijitali ambapo vijana wengi wanaweza kupata kila aina ya taarifa kutoka kwa mitandao ya kijamii na majukwaa ya mtandaoni ambayo ni vigumu kudhibiti au kuhakiki, kuna uwezekano mkubwa kwamba tayari wameishapokea aina fulani ya taarifa kuhusu kondomu—iwe ni sahihi au si sahihi.
Kwa hivyo, ni wajibu wetu kuwafahamisha vijana kikamilifu juu ya ukweli unaohusu uzazi wa mpango:

Hii inapaswa kutufanya tutafakari upya elimu ya ujinsia ambayo inazingatia matumizi ya uzazi wa mpango.

Ni vyema kutambua kwamba, kinyume na utangazaji wa kondomu, wataalam 150 wa UKiMWi duniani waliungana ili kutetea mbinu ya kuzuia maambukizi ya VVU/UKiMWi iliyo na msingi na yenye ushahidi kwa kutumia njia ifuatayo: Jizuie, Uwe mwaminifu/punguza washirika, Tumia Kondomu,24- kwa utaratibu huo.

Katika Lancet,25 “Watia saini hawaamini kuwa ni sera nzuri ya afya ya umma kutoa kipaumbele sawa kwa ujumbe mmoja (matumizi ya kondomu) kwa vijana ambao hawajaanza kujamiiana na kwa watu wanaofanya biashara ya ngono. Ukweli wote unapaswa kuwasilishwa lakini programu za kutoshiriki ngono na kadhalika (‘abstinence plus’ (SRR) lazima ziwe ‘kituo cha kujiepusha’” na sio tu programu zinazoweka taarifa za kondomu pamoja na kujizuia katika kiwango sawa. Hii ni muhimu ili kuepuka utelezi unaoletwa na fidia ya hatari.”26

Mafundisho ya Kiujumla kuhusu Idhini

Elimu ya ridhaa inachukulia kwamba wakati vijana wengi zaidi wataelewa na kuwa na ufahamu wa idhini na jinsi ya kuheshimu mipaka ya maneno ya wenzao, hii itapunguza matukio ambayo mipaka ya ngono inavukwa. ingawa kufundisha vijana kuhusu kufahamu idhini ni muhimu, yenyewe haitoshi.

Tabia haiwi na manufaa kwa vijana kwa sababu tu washirika wote wanaohusika wamekubaliana. Katika mienendo tata ya mahusiano na hali halisi ya maisha, mtu anaweza akakubaliana na kitu hata dhidi ya hukumu yake bora. Kwa kuzingatia (ukosefu wa) nyurobiolojia uwezo wa akili ya kufanya maamuzi ya busara, kutathmini hatari na kutabiri matokeo ya matendo yao na vilevile hamu yao inayochochewa na wasiwasi wa kukubalika na kumilikiwa, vijana wanaweza kujikuta wakikubali kushiriki katika jambo ambalo si zuri kwao au kwa wenzi wao.

Kwa hivyo, elimu ya ridhaa yenye ufanisi inahitaji kuangazia kigezo chenye lengo la kutathmini kama tabia fulani ni chanya au yenye madhara—na hiyo inafanya maadili ya ufundishaji kuwa sehemu ya lazima ya elimu yoyote ya ujinsia ambayo inazingatia ustawi kamili wa vijana. Uamuzi wa kujamiiana unapaswa kujumuisha taarifa za kweli kuhusu mipaka yenye afya ya kihisia, kimwili na kisaikolojia, kwa kuzingatia fadhila za ulimwenguni pote za uadilifu, upendo na heshima (kwa mtu binafsi na wengine) pamoja na sifa za kujidhibiti, uwajibikaji na ustahimilivu. Zaidi ya hayo, inafaa kujumuisha haki za wazazi kuwaelimisha watoto wao kuhusu maamuzi na mipaka ya ngono kulingana na maadili ya familia na imani zao.

Je, basi, ni mbinu gani inayowajibika zaidi: kufundisha upunguzaji wa hatari kwa vijana (SRR) hadi wawe na uwezo wa kuelewa kikamilifu matendo yao au kuondoa hatari (SRA), kwa sababu bado hawajakomaa?

Matokeo ya Utafiti Yanaunga Mkono Kutoshiriki Ngono

Kuna ushahidi unaoonyesha kwamba elimu ya ujinsia kwa vijana inayo wataarifu kujizuia na shughuli zote za ngono (mpaka ndoa) ndiyo njia salama na bora zaidi yenye asilimia 100 ya kujilinda kutokana na matokeo mabaya ya mwili, kihisia na kisaikolojia.

Kutoshiriki ngono ni kuwajibika

Wakati wa maisha yao ambapo vijana bado hawana uwezo kamili wa kutathmini kwa usahihi hatari na matokeo yanayotarajiwa, wanapaswa kufundishwa kuepuka hatari badala ya kupunguza hatari.

Watu waliolewa pombe hawawezi kabisa kufanya maamuzi ya busara kwa sababu utendaji wao umeharibiwa na athari za pombe. Je, ni salama zaidi kwa hawa walevi—na wengine—kuwafundisha jinsi ya kufunga mikanda vizuri wanapoendesha gari (kupunguza hatari) au kuwaelekeza wasiendeshe kabisa (kuondoa hatari)? Kwa hakika, wanapaswa kufahamishwa kuhusu mikanda ya usalama, lakini jambo la kuwajibika zaidi ni kuwaelimisha wasiendeshe magari wakiwa wamekunywa pombe.

Kama watu wazima—wazazi na/au waelimishaji—ni wajibu wetu kuhakikisha watoto/vijana wetu wanaepuka hatari ya ngono kabisa. Wao ni wa thamani sana kwetu kuwaruhusu kucheza kamari na maisha yao na ustawi wao kijinsia.

Kutoshiriki ngono ni muhimu

Kwa vile changamoto za afya ya akili wanazokumbana nazo vijana siku hizi zinaongezeka,27 kutoshiriki ngono kwa sasa ni chaguo muhimu na lenye busara kubwa kwa vijana. Sio tu njia ya kujikinga na kuzuia magonjwa ya zinaa na mimba zisizo halali, bali pia inalinda ustawi wa hisia na akili za vijana.

Kemikali zinazotolewa katika ubongo wakati wa shughuli za ngono hujenga uhusiano wa kihisia kati ya wenzi wa ngono, na kuvunja vifungo hivi kunaweza kusababisha mfadhaiko na kufanya iwe vigumu kwao kuungana na mtu mwingine, kama vile wenzi wao wa maisha, siku zijazo.29

Licha ya talaka kuongezeka, vijana bado wana matarajio makubwa ya kuoana na kuwa na familia huku vijana 8 kati ya 10 wanatamani kuolewa/kuoa na kupata watoto.32 Kwa hiyo vijana wanapaswa kufahamishwa kwamba kutoshiriki ngono hadi ndoa kunaweza kuongeza nafasi zao za kupata maisha bora na ubora wa ndoa.

Juu ya kutoshiriki ngono na ndoa ya baadaye:

Kutoshiriki ngono ni kitu halisi

Kuna baadhi ya wanaoona kutoshiriki ngono ni dhana ya kizamani na wanadai kuwa kufundisha vijana kufanya hivyo ni jambo lisilowezekana, iwe kwa sababu ya homoni, malezi ya familia, hali halisi au uzoefu uliopita. Hata hivyo, ukweli unapendekeza vinginevyo.

Programu za elimu ya kutoshiriki ngono zilizoundwa vyema na zilizotekelezwa vyema zimeleta matokeo yanayoonyesha vijana hawaanzi mapema kushiriki ngono, kuna upungufu wa kushiriki ngono mapema33, na kwa muda mrefu vijana wanapunguza kushiriki ngono nje ya ndoa.34

Wanafunzi huwa na tabia ya kukadiria kupita kiasi kwamba wenzao wanashiriki ngono, wanatumia dhana hii potofu kuhalalisha sababu yao wenyewe kushiriki ngono; kwa kweli, wahojiwa wengi walikuwa na mitazamo ya kihafidhina ya kijinsia.35 Kwa maneno mengine, kutoshiriki ngono inawezakana kuwa jambo la kawaida zaidi kuliko tunavyofikiri na matarajio ya kweli katika mitazamo na tabia za vijana. Utafiti kuhusu elimu ya kutoshiriki ngono, hasa kwa wale walioahidi kujizuia kutoshiriki ngono kabla ya ndoa, ulionyesha mafanikio bora kitaaluma.36

Hakuna Majuto® inashikilia mtazamo wa kutoshiriki ngono hadi wakati wa ndoa kwani ndio uamuzi bora kiafya kwa kila mmoja. Huu, ndio ujumbe ambao unafunzwa ulimwenguni kote pamoja na tabia zingine hatari kama vile unywaji pombe, dawa za kulevya, kuzusha ghasia; kuepuka tabia zote mbaya na hatari – ikiwemo, vitendo vya kushiriki ngono nje ya ndoa - kulinda mustakabali wetu kwa kuwa na uhuru mkubwa wa kudumisha urafiki, malengo, ndoto na hata afya nzuri.

Kwa vijana ambao wameisha shiriki ngono tayari, kuwasaidia kufanya ahadi upya ya kutoshiriki ngono, inawapatia nguvu na kuwawezesha sana na wanagundua uhuru mpya kuhusu ngono.

Kusonga Mbele

Hakuna Majuto® inaamini kwa wakati huu njia bora ya elimu ya ujinsia, ni kujenga ndani ya vijana wetu akili za busara juu ya kushiriki ngono. Elimu ya ujinsia ambayo ni ya utafiti, inayowajibika, inayofaa na ya kweli kwa vijana ni ile inayozingatia kukua kwao na mahitaji yao, ili waweze kupewa mwongozo unaofaa kwa umri wao na wafanye maamuzi ya busara kuhusu ngono. inajumuisha kuwafundisha kuchukua mbinu ya kuepuka au kuondoa hatari. Mtazamo kama huo hatimaye huleta matokeo bora zaidi kwa afya ya muda mfupi na muda mrefu na ustawi wa vijana wetu.37

Kutoshiriki ngono hadi wakati wa ndoa hakuwezekani – vijana watashiriki tu.

Elimu ya kutoshiriki ngono ni ya kushurutishwa – tunastahili kuacha vijana wajiamulie wenyewe.

Elimu ya kutoshiriki ngono haina wajibu – vijana lazima wafunzwe ‘kujikinga’.

Elimu ya kutoshiriki ngono ni ya kimaadili– hatupaswi kuwalazimisha wengine na maadili yetu.

Ingawa kutoshiriki ngono na usafi wa kijinsia ulikubaliwa kwa urahisi na hata kukumbatiwa katikati ya miaka 1980 na 1999, si ujumbe rahisi siku hizi kwa sababu vijana wetu wanakabiliwa na maoni tofauti juu ya ngono. Kuna kukubalika zaidi kwa tabia ambazo hapo awali zilizingatiwa kuwa zisizo za adili— ngono kabla ya ndoa, kuishi pamoja, kutazama ponografia, ushawishi wa jinsia na hata uhusiano wa kimapenzi (mahusiano ya wazi ya mtu au ya kimapenzi na zaidi ya mtu mmoja kwa wakati mmoja).

Zaidi ya hayo, vyanzo maarufu vya habari na wataalamu39 wanaripoti kila mara kwamba elimu ya kutoshiriki ngono imeshindwa.40 Kabla hatujagubikwa na taarifa hizi, ifahamike kuwa kila mara kuna upendeleo wa kibinafsi na kisiasa linapokuja suala la utafiti huo. Kwa hakika, nyingi za ripoti hizi zinakubali kwamba programu za kutoshiriki ngono pekee zimekuwa na matokeo chanya na tunao utafiti mpya wa kuthibitisha hilo.37

Hata hivyo, kufundisha kujizuia na usafi wa kijinsia pekee haitoshi. Dk. Juli Slattery alisema: “Hakuna aina yoyote ya ‘elimu ya ngono’ ambayo hatimaye itawazuia vijana kujihusisha na ngono. Tunaishi katika ulimwengu ambamo majaribio ya ngono, kutazama maonyesho ya ngono waziwazi, na kujihusisha na ponografia yamekuwa kanuni zinazokubalika. Tuna utamaduni unaoruhusu ngono na ulio wazi unaolenga vijana na watu wazima. Ongeza kwa hilo athari za simu mahiri, teknolojia ya utiririshaji, na kucheleweshwa kwa ndoa una mapishi yenye sumu ambayo inaonekana kama kwamba haiwezekani kupingwa.

Tuwawezesheje vijana wetu kuishi katika ulimwengu wao ulio mgumu? Mbinu Kamili kwa Elimu ya Jinsia Kama wawezeshaji wa Hakuna Majuto®, tunahitaji kudumisha ufundishaji bora, unaofafanuliwa na utafiti, uwajibikaji, unaofaa na wa kweli, na kuondokana na uwasilishaji wa aibu na unaoegemezwa na hofu. Mipango ya kutoshiriki ngono imeathiri vyema vijana wengi kwa sababu hatufundishi tu kuacha ngono hadi ndoa na kuchelewesha shughuli za ngono bali kuwawezesha vijana kufikiria maisha yao ya baadaye wakiwa na malengo ya muda mrefu, kujenga sifa chanya za tabia na kujenga mahusiano bora yenye afya. ingawa programu hizi hazizingatii kila kitu, hakika zitasaidia katika kuongeza uwezekano wa kufanya uchaguzi mzuri na kujenga mahusiano yenye afya, ambayo pia yanaongeza uwezekano wa familia na ndoa imara—ambayo ndiyo nyenzo muhimu zaidi ya ujenzi wa taifa.

Pia tunahitaji kuondokana na kuchanganyikiwa na kukatishwa tamaa kunakosababishwa na jumbe zenye dosari kutoka kwa programu za kujiepusha na ngono kama vile ahadi ya “ngono kuu” na ndoa yenye furaha ukijiepusha; au ujinsia wako (kama kitufe cha “kuwasha/kuzima”) unapaswa kulala hadi uolewe; au matokeo ya kujamiiana kabla ya ndoa hayawezi kutenduliwa (mafundisho yanayotegemea hofu); au usafi ni suala la ambao hawajaoa/kuolewa tu.

Shinikizo na mapambano ya usafi wa kijinsia ni magumu kuliko tu kutoshiriki ngono. Usafi wa kijinsia ni zaidi ya tendo unalolifanya, usafi unakufafanua wewe ni nani! inaweza kuonyeshwa na kile unachofanya na mwili wako (kutoshiriki ngono), lakini hatimaye mizizi yake iko ndani ya akili yako, moyo wako na nafsi yako. Majaribu yetu hayatufafanui. Tunahitaji kuwafundisha vijana kwamba ingawa hatuwezi kudhibiti kile kinachoingia akilini mwetu, tunaweza kuamua ni kitu gani kitakachobaki.

Kujizuia na usafi wa kijinsia bado ni ujumbe muhimu. Thamani ya kweli ya chaguo la vijana haiko katika thawabu ya ndoa na ngono kubwa katika siku zijazo, lakini malezi ya tabia chanya, kujistahi na utambulisho ambao utawapatia uwezo wa kukataa ushawishi mbaya, tabia mbaya za hatari, naam, hata kutoshiriki ngono kabla ya ndoa. Usafi wa kijinsia unatokana na ufahamu wakujitambua kwamba wewe ni nani.

Wewe ni wa kipekee wewe - kama mwanamume au mwanamke - mzima, wa thamani, na sifa za kipekee, uliyeumbwa ili uwe na mahusiano bora yenye afya..

Tunawahimiza vijana kutia saini kadi ya ahadi kama ishara ya nje ya kujitolea kwao Kutoshiriki ngono na usafi. Utafiti wa muda mrefu uliofanywa nchini Malaysia 41umeonyesha karibu 92% ya washiriki ambao walitia saini ahadi ya kutoshiriki ngono (hadi miaka 7) wametimiza ahadi yao. Takwimu chanya zinaonyesha kuwa wakipewa ufahamu, maarifa na changamoto ya upole, vijana wanapewa uwezo wa kufanya uchaguzi wa hekima, na ahadi ya kutoshiriki ngono ni njia rahisi lakini yenye nguvu ya kuwasaidia kutenda na kufuata uchaguzi walioufanya.

Hata hivyo, ahadi na programu zozote za muda mfupi hazina vifaa kamili vya kuwasaidia vijana wetu kuvinjari kupitia na kusimama dhidi ya shinikizo za ndani na nje zinazowakabili. Tunahitaji wazazi, washauri na wadau katika wizara na shule za vijana kuendelea kufundisha na kutoa mfano mzuri kanuni ambazo zitasaidia vijana wetu kukuza elimu ya ngono, na kuwawezesha kufanya uchaguzi maishani ambao hauna majuto wala kuomba msamaha.

Mtaala wa Hakuna Majuto® utakuwa na athari kubwa kwa vijana iwapo utawajumuisha washirika kusukuma ujumbe huu. iwapo ujumbe unaoendeleza dhana kuwa kutoshiriki ngono hadi siku ya ndoa ni mwafaka, huwezi tu kutumia kauli mbiu za ‘sema tu hapana’ ama mara moja moja madarasa ya elimu afya kuhusu magonjwa ya zinaa. Lazima elimu hiyo ijumuishe mambo mengi na kuimarishwa kwa njia mbali mbali kwa kipindi cha muda mrefu, shuleni na nyumbani. Familia, shule, jumuia za kidini, mashirika ya vijana, serikali, sehemu za biashara, na vyombo vya habari lazima wadau hawa wote wafanye juhudi za makusudi, shirikishi na makini ili vijana wajenge tabia ya kuwa waaminifu, wafanyakazi waadilifu, majirani wema, wenzi wa ndoa na wazazi wanaojali na kuwa wananchi wanaowajibika.

ikiwa wewe ni mzazi anayejali, mwalimu, ama mfanya kazi wa vijana, zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo unaweza ukatekeleza:

Wazazi

Hakuna anayemfahamu mwanao kama wewe, na hakuna “mtaalamu” ambaye anaweza kuwasiliana naye kuhusu maadili yako bora kuliko wewe. Yanapogusia masuala ya mwanao wewe ndiye mtaalamu!

Vijana wanataka kuhakikishiwa kuwa wazazi wao wanaelewa yale wanayoyapitia. Muunganiko wa mzazi-mwana pamoja na matarajio yaliyobainika ni njia mojawapo ya kupunguza aina zote za shughuli za hatari42

Ni muhimu kwa wazazi na waelimishaji kuwa tayari kuwajibu thabiti vijana yale maswali magumu, lakini halali, wanayoulizwa kuhusu ngono, mapenzi na mahusiano kwa njia inayokuza maamuzi yanayofanyika kwa sababu nzuri, maadili chanya na hatimaye maisha yajayo yenye afya bora.

Shule

Wakati shule zinapofundisha elimu ya tabia nzuri kwa umakini, thabiti na kwa kina, tabia ya wanafunzi inaboreka, shule inakuwa jamii ya kistaarabu, na hata utendaji wa kitaaluma unaboreka.

Mashirika ya kijamii

Huu ni mpango wa elimu kuhusu ngono ambao unapiga jeki kutoshiriki ngono kabla ya ndoa. Hakuna Majuto ni:

Elimu ya afya

Hakuna Majuto® inafunza kuwa ngono kabla ya ndoa inaathari mbaya kwako na kwa wengine. Ni tishio kwa afya ya vijana, ikiwemo mimba za mapema na athari zake (watoto wanapata watoto, mamilioni ya watoto wanaavya mimba duniani kote kila mwaka), magonjwa ya zinaa na athari za kiafya za muda mrefu kama ugumba.

Ingawa mipira ya ngono (kondomu) inaweza kupunguza hatari za vitendo vya ngono kabla ya ndoa, hatari nyingine za afya zinasalia. Bila kujali mwelekeo wa kijinsia au mwenzi wa mtu ni nani, njia bora ya vijana kuepuka magonjwa ya zinaa na Ukimwi ni kutoshiriki ngono hadi kwenye ndoa ya uaminifu ya mwenzi mmoja.

Therefore, No Apologies addresses the question of “How far is too far?” by giving clear guidelines to help young people draw boundaries in physical intimacy.

Elimu ya mahusiano

Ngono ni zaidi ya kukutana kimwili tu. inahusisha sehemu zote za mwanadamu – ubongo, mwili, moyo na nafsi. Kwa hivyo baadhi ya athari za ngono ya mapema ni pamoja na kuathiriwa kihisia na uwezekano wa kuwa na mahusiano mabaya siku za baadaye.

Kushiriki ngono kwa vijana ambao hawajaoana kuna athari za kisaikolojia mbaya sana. Ngono salama hailindi dhidi ya athari za kihisia za ngono kabla ya ndoa. Vitendo vya kuishi pamoja kama awamu ya majaribio ya ndoa hudhoofisha hadhi ya uthabiti wa ndoa imara-kujitoa.

inafunza vijana maana ya upendo [Mahaba] – ni zaidi ya hisia lakini inayomjali mwenzako zaidi ya ubinafsi. Ngono sio sawa na upendo (mahaba); kwa kweli, kusubiri hadi kwenye ndoa ni ishara ya upendo wa kweli na huongeza uhusiano thabiti na uliokomaa. Jambo la maana kuhusu elimu ya mahusiano ni kufundisha mipaka na mbinu za kukataa ili kukabiliana na shinikizo zitokanazo kwa vijana wa rika lao kuhusika kwenye vitendo vya ngono na tabia nyingine hatarishi.

Elimu ya tabia

Sexual behavior is determined by values rather than by mere knowledge. Therefore, No Apologies educates young people about the moral dimensions of sexual conduct and provides them with the skills, strategies, and strength of character to apply core ethical values of respect, responsibility, and self-control in the sexual domain.

inasaidia kupanua mawazo ya kimaadili ya kijana yanayohitajika ili kutambua kwamba kushiriki ngono ya kujikinga si tendo la kuwajibika. Inampatia kijana uwezo wa kufikiria na hata kuchuja jumbe mbaya ambazo hupeperushwa na vyombo vya habari kuhusu ngono, mapenzi na mahusiano. inafunza kuhusu ubikira, ambayo ni zaidi ya kutoshiriki ngono lakini mtindo wa maisha ambao unakumbutia usafi wa mawazo, moyo na mwili.

Mtaala huu unachochea fikara na unatumia takwimu iliyofasiriwa kwa uangalifu na hoja za kimaadili ili kuwaongoza vijana kufanya maamuzi sawa kwenye masuala ya ngono. Unafundisha vijana kanuni ya kuwa ni kutowajibika kiadili na kuchukua hatari kubwa zisizo za lazima kwa ustawi wa kimwili, kihisia, au kiroho kwao na kwa mtu mwingine wanaposhiriki ngono nje ya ndoa. Ujuzi wa kufanya maamuzi hufunzwa ili vijana waweza kuchukua uamuzi mwema unaokwenda sambamba na maadili yao yanayoonyesha tabia njema licha ya shinikizo la wa rika lao na ushawishi wa vyombo vya habari.

La muhimu zaidi, mpango huu unawasaidia vijana kufanya maamuzi mema kuzingatia Maisha yao ya mbeleni. Wakiwa na malengo ya muda mrefu na maono ya ndoa wana sababu ya kuweka akiba tendo la ngono kwa yule watakayeoana naye siku za baadaye. Wanafunzwa thawabu za kusubiri – sasa na hata baadaye – na kuwa mambo yote mazuri yanafaa kungojewa.

“Wakati bora wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita. Wakati mwingine bora ni sasa.”
– Methali ya Kiafrika

Wakati wowote kijana hajachelewa kufanya uamuzi mzuri kusubiri kufanya ngono hadi wakati wa ndoa. Kupitia mpango huu (program hii), mshirikishi utakuwa na fursa ya kuwasaidia vijana kukutana na ukweli ambao utawaongoza mahali papya na pazuri siku za baadaye, ili waishi maisha yao bila majuto.

Facilitating No Apologies workshops is life-changing!

Mpango huu hautawapa tu wanafunzi wako changamoto, bali utakupa changamoto wewe pia. Kila mara vijana wanatazama kama watu wazima wanashikilia na kutetea kanuni zinazoakisi dhamira ya kifalsafa ya kujitolea kudumisha kutoshiriki ngono hadi kwenye ndoa na uaminifu katika ndoa.

This field is for validation purposes and should be left unchanged.

Nitawasilisha ukweli mtupu kuhusu kuzuia (kutoshiriki ngono) badala ya kuingilia kati kuondoa hatari (kuzuia kupata mimba/mipira (kondomu)/kuavya mimba), kuepuka hatari za ngono badala ya kupunguza hatari za ngono.

Ninajitolea kuhusika moja kwa moja katika kuwaongoza wengine kwenye kiwango cha tabia ambayo sio tu inawezekana kufikiwa lakini pia italeta matokeo ya kuridhisha na yenye afya bora – bila kujali kile ambacho utamaduni unaamuru

Nitaepuka kupigia debe na hata kugawa mipira ya ngono ili nisichanganye ujumbe wa kutoshiriki na ujumbe wa ngono salama, na kudhoofisha uwezo wa kijana katika mchakato huo.

Ninakubali kuwa sitatumia nyenzo za picha mbaya ambazo zitawatatiza washirika ama kuwadhalilisha.

Nitaweka kiwango cha tabia (kutoshiriki ngono hadi ndoa, uaminifu kwenye ndoa) nikianza na maisha yangu.

Ninajitolea kuonyesha sifa za tabia nzuri kama vile uwajibikaji, heshima, uadilifu, ujasiri, kujithibiti, na uaminifu, nikijitahidi kuwafunza vijana.

Nitaheshimu hakinakili ya shirika la Focus on the Family kwa kutokuchapisha nakala za Hakuna Majuto® ama kuwaruhusu washirika wengine kufanya hivyo bila ya ruhusa

Clear Signature
Jina :(Inahitajika)

LOG IN

Ishi Maisha Yako Bila Kuomba Msamaha